Nini kinakusumbua, dhambini ukajitia

unafanya ukijua, kuwa hiyo ni hatia

Ni vyema ukaradua, kwa Ilahii kutubia

kwanini hujaamua, maasi kuyakimbia

 

Ninini kinakughuri, ukasahau ya kheri

Hivi hunayo habari, kuhusu ile safari

Hebu ifunge dhamiri, kuyaandama mazuri

usichanganye uturi, na uchafu wa kiburi

 

Tazama wanadondoka, waloishi kwa kutamba

Tazama wanatoweka, wanene pia wembamba

Bado hatujazinduka, twaasi tukijigamba

Hebu tubia hakika, Rudi Sasa kwa Muumba

 

WRITER – ALI HILAL

Categorized in: